Deuteronomy 28:3-8
3 aUtabarikiwa mjini na utabarikiwa mashambani. 4 bUtabarikiwa uzao wa tumbo lako, na mazao ya nchi yako na wanyama wako wachanga wa kufugwa, yaani ndama wa makundi yako ya ng’ombe, na wana-kondoo wa makundi yako. 5Kapu lako na vyombo vyako vya kukandia vitabarikiwa. 6 cUtabarikiwa uingiapo na utabarikiwa utokapo. 7 d Bwana atasababisha adui wainukao dhidi yako kushindwa mbele yako. Watakujia kwa njia moja lakini watakimbia mbele yako kwa njia saba. 8 e Bwana ataagiza baraka juu ya ghala zako na juu ya kila kitu utakachogusa kwa mkono wako. Bwana Mwenyezi Mungu wako atakubariki katika nchi anayokupa.
Copyright information for
SwhKC